Wengi tunasali Ibada Takatifu ya Misa.
Wewe pia nadhani unahudhuria Misa walau katika Dominika.
Lakini, umewahi kujiuliza maswali haya:
· Misa ni nini?
· Kwa nini tunahudhuria Misa?
· Misa ilianza lini?
Labda, ukiweza kuwaza maswali hayo na kuyajibu vizuri,
Msimamo wako kuhusu Misa utakuwa sahihi zaidi.
*************
Misa yote ni sala.
· Ni sala kubwa kuliko zote.
· Ni sala yenye utajiri kuliko zote.
· Ni sala iunganishayo watu wengi zaidi.
· Ni sala ya hisia zote - hudhuni, uchungu, furaha, Ibada, upendo, shukrani, maombi n.k.
· Ni sala ya Injili - ni Agizo la Yesu, ni sadaka ya Yesu, ni mazungumzo na Yesu, ni muungano na Yesu.
*************
Misa ni sadaka ya Yesu pale msalabani:
· Ni sadaka kubwa kuliko zote, kwani ni sadaka ya upendo kamili wa Mungu.
· Ni sadaka ambapo Mungu alimtoa mwanaye wapekee afe ili sisi tupone.
· Ni sadaka ambapo Mungu anamtoa mwanaye. Naye alikufa kwa ajili ya wote wa zamani, wa sasa na wa siku zote zijazo.
· Ni sadaka ya upendo wa Mungu.
· Je! Upendo wa Mungu una mwanzo? Mwisho Je?
· Hivyo ni Misa Takatifu ni sadaka ya milele...
· Tuunganikapo na Kristu katika sadaka hii, sisi tulio wa muda tunaungana na ya milele.
**************
Kiini cha Ukristu ni mapendo ya Kristu kwa wanadamu.
Kiini cha sadaka ya Misa ni Ekaristi Takatifu.
· Ekaristi Takatifu ni Kristu aliye Hai.
**************
Ekaristi Takatifu ni mapendo ya Kristu kwa wanadamu.
Yesu mwenyewe anajitoa sadaka kwa wanadamu, kwa namna ile ile aliyojitolea kuteswa na kufa pale msalabani.
Yeye mwenyewe anakuwa chakula na kinywaji cha roho kwa waumini wanaompokea.
****************
“Katika karamu ya mwisho Bwana Yesu ametunga sadaka ya Ekaristi kusudi sadaka ya msalaba iendelee siku zote mpaka atakaporudi. Aliliachia kanisa lake ukumbusho wa kifo chake na ufufuko wake kama chemchemi ya utakatifu, ishara ya umoja, na alama ya upendo; tena karamu ambayo Kristu ni chakula cha roho na mtu anajazwa na uzima wa Mungu akiahidiwa heri ya milele” (Mtaguso wa Pili wa Vatikani:47)
***************
Kumbe misa ni sadaka ya pekee!
Ni sadaka - ya upendo wa Mungu,
· iliyokamilisha sadaka zote za zamani, (“mimi sikuja kuitangua torati, bali kuikamilisha”).
· Ni sadaka ya pekee ambapo yeye mwenyewe (Kristu) ni kuhani (atoaye sadaka), altare (juu yake sadaka), altare (juu yake sadaka imewekwa) na mwanakondoo (atolewaye sadaka).
Tafakari sala hii:
“Kweli ni vema na haki tukutukuze kila wakati, Ee Bwana, lakini hasa wakati huu, kwa shangwe kubwa zaidi, kwa kuwa Kristu ametolewa sadaka awe pasaka yetu. Yeye alipoutoa mwili wake msalabani. Naya anapojitoa kwa ajili ya wokovu wetu, yeye mwenyewe alijifanya kuwa kuhani, altare na mwanakondoo. Na kwa sababu hiyo, Watu wote wanaitukuza sikukuuu ya Pasaka kwa furaha kubwa popote duniani. Nao Malaika wote wa Mbinguni wanaimba wimbo wa kukutukuza, wakisema bila mwisho:”
(Utangulizi - sala ya Ekaristi- Pasaka V)
Wewe pia nadhani unahudhuria Misa walau katika Dominika.
Lakini, umewahi kujiuliza maswali haya:
· Misa ni nini?
· Kwa nini tunahudhuria Misa?
· Misa ilianza lini?
Labda, ukiweza kuwaza maswali hayo na kuyajibu vizuri,
Msimamo wako kuhusu Misa utakuwa sahihi zaidi.
*************
Misa yote ni sala.
· Ni sala kubwa kuliko zote.
· Ni sala yenye utajiri kuliko zote.
· Ni sala iunganishayo watu wengi zaidi.
· Ni sala ya hisia zote - hudhuni, uchungu, furaha, Ibada, upendo, shukrani, maombi n.k.
· Ni sala ya Injili - ni Agizo la Yesu, ni sadaka ya Yesu, ni mazungumzo na Yesu, ni muungano na Yesu.
*************
Misa ni sadaka ya Yesu pale msalabani:
· Ni sadaka kubwa kuliko zote, kwani ni sadaka ya upendo kamili wa Mungu.
· Ni sadaka ambapo Mungu alimtoa mwanaye wapekee afe ili sisi tupone.
· Ni sadaka ambapo Mungu anamtoa mwanaye. Naye alikufa kwa ajili ya wote wa zamani, wa sasa na wa siku zote zijazo.
· Ni sadaka ya upendo wa Mungu.
· Je! Upendo wa Mungu una mwanzo? Mwisho Je?
· Hivyo ni Misa Takatifu ni sadaka ya milele...
· Tuunganikapo na Kristu katika sadaka hii, sisi tulio wa muda tunaungana na ya milele.
**************
Kiini cha Ukristu ni mapendo ya Kristu kwa wanadamu.
Kiini cha sadaka ya Misa ni Ekaristi Takatifu.
· Ekaristi Takatifu ni Kristu aliye Hai.
**************
Ekaristi Takatifu ni mapendo ya Kristu kwa wanadamu.
Yesu mwenyewe anajitoa sadaka kwa wanadamu, kwa namna ile ile aliyojitolea kuteswa na kufa pale msalabani.
Yeye mwenyewe anakuwa chakula na kinywaji cha roho kwa waumini wanaompokea.
****************
“Katika karamu ya mwisho Bwana Yesu ametunga sadaka ya Ekaristi kusudi sadaka ya msalaba iendelee siku zote mpaka atakaporudi. Aliliachia kanisa lake ukumbusho wa kifo chake na ufufuko wake kama chemchemi ya utakatifu, ishara ya umoja, na alama ya upendo; tena karamu ambayo Kristu ni chakula cha roho na mtu anajazwa na uzima wa Mungu akiahidiwa heri ya milele” (Mtaguso wa Pili wa Vatikani:47)
***************
Kumbe misa ni sadaka ya pekee!
Ni sadaka - ya upendo wa Mungu,
· iliyokamilisha sadaka zote za zamani, (“mimi sikuja kuitangua torati, bali kuikamilisha”).
· Ni sadaka ya pekee ambapo yeye mwenyewe (Kristu) ni kuhani (atoaye sadaka), altare (juu yake sadaka), altare (juu yake sadaka imewekwa) na mwanakondoo (atolewaye sadaka).
Tafakari sala hii:
“Kweli ni vema na haki tukutukuze kila wakati, Ee Bwana, lakini hasa wakati huu, kwa shangwe kubwa zaidi, kwa kuwa Kristu ametolewa sadaka awe pasaka yetu. Yeye alipoutoa mwili wake msalabani. Naya anapojitoa kwa ajili ya wokovu wetu, yeye mwenyewe alijifanya kuwa kuhani, altare na mwanakondoo. Na kwa sababu hiyo, Watu wote wanaitukuza sikukuuu ya Pasaka kwa furaha kubwa popote duniani. Nao Malaika wote wa Mbinguni wanaimba wimbo wa kukutukuza, wakisema bila mwisho:”
(Utangulizi - sala ya Ekaristi- Pasaka V)
Maisha ya Yesu na sadaka ya Misa
Yohana 4: 13 - 14
“Yesu akamjibu (mwanamke Masamaria), kila anayekunywa maji haya (ya kisima cha Yakobo ) ataona kiu tena. Lakini atakeyekunywa maji nitakayompa, hataona kiu milele. Maji nitakayompa yatakuwa chemichemi ya maji ya uzima na kumpatia uzima wa Milele’’
Yohana 6 : 35
“Yesu akawaambia (Wayahudi waliojaa sinagogi la Kafarnaum) Mimi ndimi mkate wa uzima. Anakuja kwangu hataona njaa; anayeniamini hataona kiu kamwe ”.
Yohana 6: 41
“. . basi Wayahudi wakaanza kunung’unika kwa kuwa alisema: Mimi ni mkate ulioshuka kutoka Mbinguni”.
Yohana 6: 50 - 51
“Huu ndio mkate ushukao kutoka Mbinguni; mkate ambao anayekula hatakufa. . Mimi ni mkate hai ulioshuka kutoka Mbinguni. Mtu yeyote akila mkate huu ataishi milele. Na mkate nitakaompa ni mwili wangu ninautoa kwa ajili ya uzima wa ulimwengu”
Yohana 6: 53
“Yesu akawaambia, kweli nawaambieni, msipokula mwili wa mwana wa mtu na kunywa damu yake, hamtakuwa na uzima ndani yenu”.
Yohana 6: 54
“Anayekula mwili wangu na kunywa damu yangu, anao uzima wa milele, nami nitamfufua siku ya mwisho”.
Yohana 6: 55
“Maana mwili wangu ni chakula cha kweli na damu yangu ni kinywaji cha kweli”.
Yohana 6: 56
“Aulaye mwili wangu na kunywa damu yangu, anakaa ndani yangu, nami nakaa ndani yake”.
Yohana 6: 57
“Baba aliye hai alinituma, nami naishi sababu yake; vivyo hivyo anilaye mimi ataishi pia kwa sababu yangu”.
Yohana 6: 58
“Basi huu ndio mkate ulioshuka kutoka mbinguni; si kama mana waliokula baba zenu, wakafa. Aulaye mkate huu atakuwa na uzima wa milele”.
Yohana 4: 13 - 14
“Yesu akamjibu (mwanamke Masamaria), kila anayekunywa maji haya (ya kisima cha Yakobo ) ataona kiu tena. Lakini atakeyekunywa maji nitakayompa, hataona kiu milele. Maji nitakayompa yatakuwa chemichemi ya maji ya uzima na kumpatia uzima wa Milele’’
Yohana 6 : 35
“Yesu akawaambia (Wayahudi waliojaa sinagogi la Kafarnaum) Mimi ndimi mkate wa uzima. Anakuja kwangu hataona njaa; anayeniamini hataona kiu kamwe ”.
Yohana 6: 41
“. . basi Wayahudi wakaanza kunung’unika kwa kuwa alisema: Mimi ni mkate ulioshuka kutoka Mbinguni”.
Yohana 6: 50 - 51
“Huu ndio mkate ushukao kutoka Mbinguni; mkate ambao anayekula hatakufa. . Mimi ni mkate hai ulioshuka kutoka Mbinguni. Mtu yeyote akila mkate huu ataishi milele. Na mkate nitakaompa ni mwili wangu ninautoa kwa ajili ya uzima wa ulimwengu”
Yohana 6: 53
“Yesu akawaambia, kweli nawaambieni, msipokula mwili wa mwana wa mtu na kunywa damu yake, hamtakuwa na uzima ndani yenu”.
Yohana 6: 54
“Anayekula mwili wangu na kunywa damu yangu, anao uzima wa milele, nami nitamfufua siku ya mwisho”.
Yohana 6: 55
“Maana mwili wangu ni chakula cha kweli na damu yangu ni kinywaji cha kweli”.
Yohana 6: 56
“Aulaye mwili wangu na kunywa damu yangu, anakaa ndani yangu, nami nakaa ndani yake”.
Yohana 6: 57
“Baba aliye hai alinituma, nami naishi sababu yake; vivyo hivyo anilaye mimi ataishi pia kwa sababu yangu”.
Yohana 6: 58
“Basi huu ndio mkate ulioshuka kutoka mbinguni; si kama mana waliokula baba zenu, wakafa. Aulaye mkate huu atakuwa na uzima wa milele”.
Zoezi:
Tafakari asehemu hizo za Injili ya Yohana, kipengele baada ya kipengele.
Baada ya kutafakari, soma Yohane 6: 35 - 58 kwa sauti. Unaiona picha halisi ya sadaka ya Ekaristi
Sali - mshukuru Yesu wa Ekaristi, kwa kutupa zawadi hii - ili tuwe naye daima.
Wewe na Ibada ya misa
Ibada ya Misa ni kama mti mzuri utoao maua na matunda mazuri. Majani na maua yake hupendeza. Watu huchuma maua yake wakapamba nyumba zao. Wengine huchuma matunda yake wakala wakashiba, tena katika matunda hupata mbengu wakazipanda zikaota miti mingine. Wakati wa jua kali, watu wengine hupata kivuli chini ya mti huo; na mvua inyeshapo, wengine hupata kinga chini ya mti huu. Nyuki nao huvutiwa na maua ya mti huu - katika maua yake wanapata vifaa vya kutengeneza asali na nta.
Fikiri: Wewe ni nani katika mti huu?
· Mtu achukuaye maua yake na kupanba nyumba yake?
· Mtu achumaye matunda na kuyala; kisha mbegu zake akazitupa bila kujali zitakapoanguka?
· Mtu achumaye matunda na kuyala; kisha mbegu zake akazipanda penye ardhi nzuri nazo zikaota kuwa miti mingine?
· Mtu apataye kivuli chini ya mti huu?
· Mtu apataye apataye kinga ya mvua chini ya mti huu?
· Nyuki apataye kutoka maua ya mti vifaa vya kutengeneza asali na nta?
· Au mtu afaidikaye na asali na nta ya nyuki?
Fikiri: Mti huu ni mali hasa ya nani?
* Nani awezaye kusema mti huu ni mali yake kati ya hao saba?
Hatima: Pata wazo kuwa Ibada ya Misa ni upendo wa Mungu.
Upendo wa Mungu ni kwa watu wote. Hivyo Sadaka ya Misa ni ya watu wote; ni moja, na atolewaye ni mmoja, ndiye Yesu Kristu. Hutupa faida za muda (kama mti ulivyokuwa katika mapato, kivuli na kinga ya mvua), pia hutupa faida zidumuzo (kama ulivyo mti katika maua na matunda). Tunda la mti huu ni Ekaristi Takatifu.
Sadaka ya Misa: Maua
Hakika Ibada ya Misa ni Ibada ya kupendeza macho na mioyo, hasa ikijumuisha tamaduni zetu (inculturation).
Fikiri vitu hivi:
· Watu wenye nia njema - matajiri waliovaa nguo nzuri na maskini zile nzuri zaidi walizonazo.
· Mapambo ya Altare na kanisa: vitambaa, maua, mishumaa n. k.
· Nyimbo nzuri zenye kupendeza ziambatanazo na vigelegele, vinanda, tarumbeta, kengele n. k.
· Maandamano ya Padre na watumishi, maandamano ya matoleo n. k.
· Sala za Liturgia zenye kugusa moyo na kuamsha moyo wa Ibada.
Vyote hivi hupendendeza; hupendeza kama ua, huvutia kama ua na wote washirikio huondoka na mioyo iliyopendezeshwa. .
Jichunguze/chunguza:
Ni kipi kinachokuvutia zaidi katika Ibada ya Misa? Ni kipi kinachowavutia watu, kwa mfano kufunga ndoa zao katika Ibada ya Misa japokuwa wao hawana mazoea ya kwenda kanisani?
***************
Sadaka ya Misa: Matunda
· Sayansi yatuambia kuwa maua hugeuka kuwa matunda hatimaye. Kile kilichowavutia watu kwa sura na harufu yake, baadaye huwa shibe yao.
· Wajao katika Ibada ya Misa hushibishwa ubinadamu wao. Ni kusanyiko la watu ambapo weupe kwa weusi, wake kwa waume, matajiri kwa maskini huwa sawa wakisoma neno moja, wakisikilizana sauti ya mmoja, wakikiri imani moja, wakipata baraka ya mmoja na kula chakula kimoja ambacho huwafanya mwili mmoja katika Mungu mmoja. Ni sadaka ya UMOJA.
· Wao katika Ibada ya Misa hushibishwa roho zao kwa neno wa Mungu (Liturgia ya Neno) na sakramenti ya Ekaristi (liturgia ya Ekaristi). Kristu aliye hai hujionyesha katika maisha yao kwa njia ya mahubiri tena huonyesha upendo wake na utashi wake wa kuwa nasi daima kwa njia ya komunio Takatifu, na huonyesha dhamiri yake ya kusamehe na kututakasa (na hakika hututakasa) kwa njia ya damu yake takatifu.
· Umungu wake huonekana: Fikiri alivyo wa ajabu huyu Yesu wa Ekaristi: Mkate mmoja - watu wengi, nchi mbalimbali, zamani, sasa na baadaye. . . Lakili Kristu ni yule yule mmoja hagawanyiki, hapungui wala hazeeki wala kuoza. . . huwepo kwa yeyote apendaye kumpokea wakati wowote, popote. . .
***************
Sadaka ya Misa: Mbegu
Mara nyingi mbegu huwapo katika tunda. Katika sadaka ya Misa pia kuna mbegu, mbegu za NENO LA MUNGU. Mpandaji mkuu ni KRISTU mwenyewe. . . . lakini anatualika wote tufaidikao na matunda pia tuwe wapandaji wasaidizi.
· KRISTU hupanda neno lake katika mioyo yetu, neno hili hukua, likaota mizizi. . . maua yakatokea na kutupendezesha mbele za Mungu na wanadamu na kuwavutia watu kwetu ambao sisi huwaelekeza kwa KRISTU.
· Matunda hutokea nasi hufaidi zaidi. Mbegu tuzipatazo kutoka katika matunda huzipanda kwa wengine . . . Je! baada ya kupanda inatupasa kusaidia palizi, kunyweshea n. k. hadi maua na matunda yapatikane? Jadili nafsini mwako.
· Watoto wetu huwaleta katika Ibada ya Misa ambapo nao kama mashamba:
1. Hutayarishwa kwa kilimo na kutiwa mbolea - mafunzo na kitubio.
2. Hupandwa - neno na sakramenti mbalimbali na
3. Hutunzwa kwa sakramenti na visakramenti mbalimbali hadi matunda yanapatikana.
· Sote sisi hushirikishwa na Kristu katika kutayarisha shamba, kupanda, kutunza mimea. . . nasi hufaidika na matunda sasa. . . na milele. . .
Sadaka ya Misa yatushirikisha sote upanzi wa Kristu:
· Sisi hupanda pamoja na Kristu.
· Sisi hutumwa kupanda pamoja na Kristu.
· Sisi pia tu udongo . . . ndani yetu mbegu hupandwa.
Kwa nini tunazungumzia sisi wala si mimi?
Jibu: Sadaka ya Misa ni ya wengi si ya mmoja. Yawahusu walio Mbinguni na walio Duniani; walio taabani vitandani na walio kuzimu; walioishi, wanaoishi na watakaoishi; waamini na wasioamini; waasi na waalimu wa kanisa; watu wote. . . ambao Kristu aliwafia msalabani. Ni sadaka KATOLIKI.
***************
Sadaka ya misa: Faraja
Yule aliyejikinga kwa jua na mvua chini ya mti alipata faraja. Ibada ya misa ni uwepo wa Mungu katika ukamili wa upendo wake, huruma yake na utukufu wake.
Kuuhisi uwepo wa Mungu hakika huleta faraja kubwa ya moyo:
· Dhambi zetu hufutika mbele ya upendo na huruma ya Mungu.
· Elimu, sayansi na Teknolojia hushushwa na kuonekana kama mawazo mazuri ya mtoto mtundu na mbunifu mbele ya babaye ajuaye yote.
· Uzito na taabu za duniani huonekana vitu vidogo sana mbele ya msalaba wa Kristu.
· Kifo kwa wakiogopao hushindwa kabisa mbele ya Kristu mfufuka aliyeyashinda mauti. Si tishio tena kwao!
· Kifo kwa wamtumainiao huwa furaha ya kueandelea kuwa naye. Misa yatudhihirishia waamini kuwa tu wake tuwapo hai pia tufapo. Tunakuwa kama fedha iliyohamishwa kutoka mfuko mmoja wa vazi kwenda mwingine. . . na bado tunabaki mali ya mwenye vazi, tena ndani yake.
· Utajiri huwa kipaji cha kusaidia maskini; na umaskini huwa shule ya kujifunza kumtegemea na kutambua upendo na huruma zake.
Ibada ya misa ni faraja kwa wote. Yeye mwenye Ibada hii alisema:
“Njooni kwangu ninyi nyote mnaosumbuka na kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha” (Mathayo 11: 28).
“Nendeni mkawambie. . . . . mambo mnayoyasikia na kuyaona:
Vipofu wanona,
Viwete wanatembea,
Wenye Ukoma wanatakaswa na
Viziwi wanasikia tena;
Wafu wanafufuliwa, na maskini wanahubiriwa habari njema,
Heri mtu yule asiyekuwa na mashaka nami”. (Mathayo 11: 4 - 6)
Fikiri furaha na faraja waipatao:
· Vipofu wanapopata tena kuona. Jiweke katika nafasi ya kipofu fulani. . . .
· Viwete wanaopata kutembea . . . jiweke katika nafasi ya kiwete mmoja wa hao - kiasi gani utarukaruka kwa furaha!?
· Mwenye ukoma anayetakaswa . . .
· Kiziwi anayepata tena kusikia . . .
· Mfu anayepata uzima tena . . .
· Maskini anayeahidiwa UTAJIRI WA MILELE ,,,
ZOEZI DOGO: TAFAKARI MATHAYO 11: 4 - 6
Tafakari asehemu hizo za Injili ya Yohana, kipengele baada ya kipengele.
Baada ya kutafakari, soma Yohane 6: 35 - 58 kwa sauti. Unaiona picha halisi ya sadaka ya Ekaristi
Sali - mshukuru Yesu wa Ekaristi, kwa kutupa zawadi hii - ili tuwe naye daima.
Wewe na Ibada ya misa
Ibada ya Misa ni kama mti mzuri utoao maua na matunda mazuri. Majani na maua yake hupendeza. Watu huchuma maua yake wakapamba nyumba zao. Wengine huchuma matunda yake wakala wakashiba, tena katika matunda hupata mbengu wakazipanda zikaota miti mingine. Wakati wa jua kali, watu wengine hupata kivuli chini ya mti huo; na mvua inyeshapo, wengine hupata kinga chini ya mti huu. Nyuki nao huvutiwa na maua ya mti huu - katika maua yake wanapata vifaa vya kutengeneza asali na nta.
Fikiri: Wewe ni nani katika mti huu?
· Mtu achukuaye maua yake na kupanba nyumba yake?
· Mtu achumaye matunda na kuyala; kisha mbegu zake akazitupa bila kujali zitakapoanguka?
· Mtu achumaye matunda na kuyala; kisha mbegu zake akazipanda penye ardhi nzuri nazo zikaota kuwa miti mingine?
· Mtu apataye kivuli chini ya mti huu?
· Mtu apataye apataye kinga ya mvua chini ya mti huu?
· Nyuki apataye kutoka maua ya mti vifaa vya kutengeneza asali na nta?
· Au mtu afaidikaye na asali na nta ya nyuki?
Fikiri: Mti huu ni mali hasa ya nani?
* Nani awezaye kusema mti huu ni mali yake kati ya hao saba?
Hatima: Pata wazo kuwa Ibada ya Misa ni upendo wa Mungu.
Upendo wa Mungu ni kwa watu wote. Hivyo Sadaka ya Misa ni ya watu wote; ni moja, na atolewaye ni mmoja, ndiye Yesu Kristu. Hutupa faida za muda (kama mti ulivyokuwa katika mapato, kivuli na kinga ya mvua), pia hutupa faida zidumuzo (kama ulivyo mti katika maua na matunda). Tunda la mti huu ni Ekaristi Takatifu.
Sadaka ya Misa: Maua
Hakika Ibada ya Misa ni Ibada ya kupendeza macho na mioyo, hasa ikijumuisha tamaduni zetu (inculturation).
Fikiri vitu hivi:
· Watu wenye nia njema - matajiri waliovaa nguo nzuri na maskini zile nzuri zaidi walizonazo.
· Mapambo ya Altare na kanisa: vitambaa, maua, mishumaa n. k.
· Nyimbo nzuri zenye kupendeza ziambatanazo na vigelegele, vinanda, tarumbeta, kengele n. k.
· Maandamano ya Padre na watumishi, maandamano ya matoleo n. k.
· Sala za Liturgia zenye kugusa moyo na kuamsha moyo wa Ibada.
Vyote hivi hupendendeza; hupendeza kama ua, huvutia kama ua na wote washirikio huondoka na mioyo iliyopendezeshwa. .
Jichunguze/chunguza:
Ni kipi kinachokuvutia zaidi katika Ibada ya Misa? Ni kipi kinachowavutia watu, kwa mfano kufunga ndoa zao katika Ibada ya Misa japokuwa wao hawana mazoea ya kwenda kanisani?
***************
Sadaka ya Misa: Matunda
· Sayansi yatuambia kuwa maua hugeuka kuwa matunda hatimaye. Kile kilichowavutia watu kwa sura na harufu yake, baadaye huwa shibe yao.
· Wajao katika Ibada ya Misa hushibishwa ubinadamu wao. Ni kusanyiko la watu ambapo weupe kwa weusi, wake kwa waume, matajiri kwa maskini huwa sawa wakisoma neno moja, wakisikilizana sauti ya mmoja, wakikiri imani moja, wakipata baraka ya mmoja na kula chakula kimoja ambacho huwafanya mwili mmoja katika Mungu mmoja. Ni sadaka ya UMOJA.
· Wao katika Ibada ya Misa hushibishwa roho zao kwa neno wa Mungu (Liturgia ya Neno) na sakramenti ya Ekaristi (liturgia ya Ekaristi). Kristu aliye hai hujionyesha katika maisha yao kwa njia ya mahubiri tena huonyesha upendo wake na utashi wake wa kuwa nasi daima kwa njia ya komunio Takatifu, na huonyesha dhamiri yake ya kusamehe na kututakasa (na hakika hututakasa) kwa njia ya damu yake takatifu.
· Umungu wake huonekana: Fikiri alivyo wa ajabu huyu Yesu wa Ekaristi: Mkate mmoja - watu wengi, nchi mbalimbali, zamani, sasa na baadaye. . . Lakili Kristu ni yule yule mmoja hagawanyiki, hapungui wala hazeeki wala kuoza. . . huwepo kwa yeyote apendaye kumpokea wakati wowote, popote. . .
***************
Sadaka ya Misa: Mbegu
Mara nyingi mbegu huwapo katika tunda. Katika sadaka ya Misa pia kuna mbegu, mbegu za NENO LA MUNGU. Mpandaji mkuu ni KRISTU mwenyewe. . . . lakini anatualika wote tufaidikao na matunda pia tuwe wapandaji wasaidizi.
· KRISTU hupanda neno lake katika mioyo yetu, neno hili hukua, likaota mizizi. . . maua yakatokea na kutupendezesha mbele za Mungu na wanadamu na kuwavutia watu kwetu ambao sisi huwaelekeza kwa KRISTU.
· Matunda hutokea nasi hufaidi zaidi. Mbegu tuzipatazo kutoka katika matunda huzipanda kwa wengine . . . Je! baada ya kupanda inatupasa kusaidia palizi, kunyweshea n. k. hadi maua na matunda yapatikane? Jadili nafsini mwako.
· Watoto wetu huwaleta katika Ibada ya Misa ambapo nao kama mashamba:
1. Hutayarishwa kwa kilimo na kutiwa mbolea - mafunzo na kitubio.
2. Hupandwa - neno na sakramenti mbalimbali na
3. Hutunzwa kwa sakramenti na visakramenti mbalimbali hadi matunda yanapatikana.
· Sote sisi hushirikishwa na Kristu katika kutayarisha shamba, kupanda, kutunza mimea. . . nasi hufaidika na matunda sasa. . . na milele. . .
Sadaka ya Misa yatushirikisha sote upanzi wa Kristu:
· Sisi hupanda pamoja na Kristu.
· Sisi hutumwa kupanda pamoja na Kristu.
· Sisi pia tu udongo . . . ndani yetu mbegu hupandwa.
Kwa nini tunazungumzia sisi wala si mimi?
Jibu: Sadaka ya Misa ni ya wengi si ya mmoja. Yawahusu walio Mbinguni na walio Duniani; walio taabani vitandani na walio kuzimu; walioishi, wanaoishi na watakaoishi; waamini na wasioamini; waasi na waalimu wa kanisa; watu wote. . . ambao Kristu aliwafia msalabani. Ni sadaka KATOLIKI.
***************
Sadaka ya misa: Faraja
Yule aliyejikinga kwa jua na mvua chini ya mti alipata faraja. Ibada ya misa ni uwepo wa Mungu katika ukamili wa upendo wake, huruma yake na utukufu wake.
Kuuhisi uwepo wa Mungu hakika huleta faraja kubwa ya moyo:
· Dhambi zetu hufutika mbele ya upendo na huruma ya Mungu.
· Elimu, sayansi na Teknolojia hushushwa na kuonekana kama mawazo mazuri ya mtoto mtundu na mbunifu mbele ya babaye ajuaye yote.
· Uzito na taabu za duniani huonekana vitu vidogo sana mbele ya msalaba wa Kristu.
· Kifo kwa wakiogopao hushindwa kabisa mbele ya Kristu mfufuka aliyeyashinda mauti. Si tishio tena kwao!
· Kifo kwa wamtumainiao huwa furaha ya kueandelea kuwa naye. Misa yatudhihirishia waamini kuwa tu wake tuwapo hai pia tufapo. Tunakuwa kama fedha iliyohamishwa kutoka mfuko mmoja wa vazi kwenda mwingine. . . na bado tunabaki mali ya mwenye vazi, tena ndani yake.
· Utajiri huwa kipaji cha kusaidia maskini; na umaskini huwa shule ya kujifunza kumtegemea na kutambua upendo na huruma zake.
Ibada ya misa ni faraja kwa wote. Yeye mwenye Ibada hii alisema:
“Njooni kwangu ninyi nyote mnaosumbuka na kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha” (Mathayo 11: 28).
“Nendeni mkawambie. . . . . mambo mnayoyasikia na kuyaona:
Vipofu wanona,
Viwete wanatembea,
Wenye Ukoma wanatakaswa na
Viziwi wanasikia tena;
Wafu wanafufuliwa, na maskini wanahubiriwa habari njema,
Heri mtu yule asiyekuwa na mashaka nami”. (Mathayo 11: 4 - 6)
Fikiri furaha na faraja waipatao:
· Vipofu wanapopata tena kuona. Jiweke katika nafasi ya kipofu fulani. . . .
· Viwete wanaopata kutembea . . . jiweke katika nafasi ya kiwete mmoja wa hao - kiasi gani utarukaruka kwa furaha!?
· Mwenye ukoma anayetakaswa . . .
· Kiziwi anayepata tena kusikia . . .
· Mfu anayepata uzima tena . . .
· Maskini anayeahidiwa UTAJIRI WA MILELE ,,,
ZOEZI DOGO: TAFAKARI MATHAYO 11: 4 - 6